Ehsan Ajiq, naibu mkuu wa Idara ya Masuala ya Kidini Uturuki ametangaza Jumanne kuwa misahafu hiyo imesambazwa katika fremu ya kampeni ya ‘Zawadi Yangu Inapaswa Kuwa Qur’ani Tukufu’ ambayo ilianzishwa mwaka 105. Katika fremu ya kampeni hiyo misahafu milioni moja imesambazwa katika nchi 80 duniani.
Ajiq ameongeza kuwa wamejitahidi kuhakikisha kuwa ujumbe wa Qur’ani Tukufu unawafikia watu katika kona zote za dunia. Aidha amesema nakala za Qur’ani ambazo wanasamabza pia zina tarjuma ya lugha 20 za maeneo muhimu ya dunia.