IQNA

Amnesty International

Jeshi la Nigeria liliwazika hai na kwa umati Waislamu

18:06 - April 22, 2016
Habari ID: 3470262
Jeshi la Nigeria liliwaua mamia ya Waislamu nchini Nigeria na kuwazika katika kaburi la umati wakiwemo baadhi waliokuwa hai mwezi Desemba mwaka jana, imefichua Amnesty International.

Katika taarifa siku ya Ijumaa, Amnesty imesema jeshi la Nigeria liliua zaidi ya Waislamu 350 wanachama wa Harakati ya Kiislamu Nigeria inayoongozwa na Sheikh Ibrahim Zakzaky. Ripoti hiyo imefichua kuwa, jeshi la Nigeria lilijaribu kuficha ushahidi wa jinai hiyo kwa kuwazika waathrika katika makaburi ya umati huku watu wa kawaida wakizuia kufika katika baadhi ya maeneo ya jinai hiyo katika mji wa Zaria jimboni Kaduna.
Ikumbukwe kuwa Desemba 12 mwaka jana, wanajeshi wa Nigeria waliwashambulia Waislamu waliokuwa katika kituo cha Kiislamu Zaria na kuwatuhumu kuwa walifunga njia ya msafara wa mkuu wa jeshi kwa njama ya kumuua.
Waislamu wa eneo hilo wamepinga vikali tuhuma hizo. Siku moja baadaye, jeshi la Nigeria lilivamia nyuma ya Sheikh Zakzaky na kumtia mbaroni sambamba na kuua mamia ya Waislamu waliokuwa wakimlinda. Katika matukio hayo mawili, mamia ya wafuasi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria waliuawa kwa umati, wakiwemo watoto wawili wa Sheikh Zakzaky. Baadhi ya duru zinadikeza kuwa waliouawa katika tukio hilo ni Zaidi ya elfu moja. Amnesty International imesema Jeshi la Nigeria jeshi la Nigeria liliwachoma moto Waislamu hai sambamba na kuteketeza nyumba na kutuma miiili katika makaburi ya umati. Ripoti hiyo imesema sit u kuwa jeshi la Nigeria lilitumia nguvu ziada dhidi ya wanawake, watoto na wanaume na kisha kuwaua kwa umati, bali pia kumefanyika njama za makusudi za kufika ukweli kuhusu jinai hiyo. Aidha Amnesty imeutaka utawala wa Rais Muhammadu Buhari kuchunguza muaji hayo ya Waislamu wasio na hatia.

3490921

captcha